Sunday, January 18, 2015

SHARE HII: WATOTO MAPACHA WALIOUNGANA KIFUANI WAFARIKI DUNIA HUKO MWANZA>>> COMMENT R.I.P KAMA UNAPENDA WATOTO


Hawa ndiyo mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana Mkoani Mara
Taarifa kutoka Mkoani Mwanza zinaeleza kuwa wale watoto mapacha waliozaliwa wakiwa wameungana katika eneo la kifua hadi tumboni, tukio lililovuta hisia za mamia ya wananchi waliofika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara  walikufa  juzi katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.
Mapacha hao ambao ni wa kike walifariki dunia wakati madaktari wa hospitali hiyo wakijiandaa kuwafanyia upasuaji kwa ajili ya kuwatenganisha.
Mama mzazi wa watoto hao, Helena Paulo (20)  ni mkazi wa Kata ya Buhare katika Manispaa ya Musoma  Mara. Alifanikiwa kujifungua kwa njia ya upasuaji (operesheni) Januari 5, mwaka huu  saa saba usiku.
Daktari katika Wodi ya Watoto ya Hospitali ya Rufaa ya Bugando  Dk. Shukuru Kibwana,  amesema walimpokea mama wa watoto hao Januari 5 na kwamba baada ya kuwafanyia uchuguzi wa kina watoto hao  ilibainika kwamba wanaweza kutenganishwa kwa sababu kila mmoja alikuwa na mfumo wake unaojitegemea wa kula na kupata hewa  hivyo kilichokuwa kimebaki ilikuwa ni matibabu  upasuaji.
“Tangu tulipowapokea watoto hawa  timu ya madaktari wa upasuaji na wataalamu wengine tulifanya kila lililowezekana kuokoa maisha ya watoto hawa  lakini juhudi hizo hazikufanikiwa kama tulivyokuwa tunategemea  kwa bahati mbaya waliaga dunia,” alisema Dk Kibwana.

No comments:

Post a Comment